Wanyongwa Indonesia kwa dawa za kulevya
Mwanasheria mkuu wa serikali nchini humo Noor Rachmad amesema raia watatu wa Nigeria na Muindonesia mmoja wameuawa kwa kupigwa risasi katika gereza la kisiwa cha Nusa Kambangan.
Mapema wiki hii mwanasheria mkuu wa serikali nchini humo amesema watu 14, wengi wao wakiwa ni wageni watanyongwa.
Serikali mbalimbali za kigeni, Makundi ya haki za binadamu na ndugu za watu hao walizitaka Mamlaka nchini Indonesia kuacha kuwaua watu hao.

Comments
Post a Comment