FAO inasaka ufadhili wa haraka kusaidia watu 385,000 Nigeria


Kwa mujibu wa taarifa ya shirika la chakula na kilimo duniani, FAO iliyotolewa leo, watu Laki Tatu na Elfu Themanini na Watano wanahitaji msaada wa pembejeo za kilimo na kujikimu kimaisha katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria ambako kuna matatizo ya uhakika wa chakula kutokana na ukosefu wa usalama.
Shirika hilo linasema kuanza shughuli za kilimo hivi sasa ni muhimu sana ili kuhakikisha kwamba watu wanazalisha chakula cha kutosha kwa mahitaji yao, ikiwa ni pamoja na wakimbizi wa ndani waliotawanywa na machafuko pamoja na jamii ambazo zinawahifadhi.

Comments

Popular posts from this blog

VYOMBO VYA HABARI VINAWAJIBU WA KUELIMISHA JUU YA MALENGO 17 YA MAENDELEO ENDELEVU

DINI YAELEZWA KUWA KICHOCHEO CHA KUTIMIZA SDGS

7 hatua kuelekea maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030