Ban ziarani California; SDGs na wakimbizi kwenye ajenda
Katibu Mkuu wa
Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, yupo ziarani Los Angeles, jimbo la Kalifonia,
Marekani, ambako anatarajiwa kukutana na viongozi katika fani ya sanaa ya
muziki na filamu, ili kujadili jinsi wanavyoweza kuunga mkono malengo ya Umoja
wa Mataifa.
Katika ziara
hiyo, Ban anatarajiwa pia kukutana na Mwenyekiti wa Kamati ya masuala ya kigeni
katika bunge la Marekani, Ed Royce.
Aidha, Katibu
Mkuu anatarajiwa kushiriki hafla ya kuwapatia makazi mapya wakimbizi, hafla
ambayo imeandaliwa na mashirika ya International Rescue Committee (IRC) na
Annenberg Foundation.

Comments
Post a Comment