Sudan Kusini yaongoza kwa kuwa na watoto wasiokwenda shule:UNICEF
Katika taarifa yake ya leo, UNICEF imesema Sudan Kusini ndiyo yenye idadi kubwa zaidi ambako zaidi ya nusu ya watoto wenye umri wa kuwa shule za msingi na sekondari hawako shuleni. Nchi ya pili ni Niger, ikifuatiwa na Sudan na Afghanistan.
Akihojiwa na redio ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi, msemaji wa UNICEF Christophe Boulierac amesisitiza umuhimu wa kutoa huduma za elimu wakati wa mizozo.

Comments
Post a Comment