Sudan Kusini yaongoza kwa kuwa na watoto wasiokwenda shule:UNICEF




Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema watoto takribani Milioni 24 walio katika nchi 22 zenye mizozo hawako shuleni.

Katika taarifa yake ya leo, UNICEF imesema Sudan Kusini ndiyo yenye idadi kubwa zaidi ambako zaidi ya nusu ya watoto wenye umri wa kuwa shule za msingi na sekondari hawako shuleni. Nchi ya pili ni Niger, ikifuatiwa na Sudan na Afghanistan.
Akihojiwa na redio ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi, msemaji wa UNICEF Christophe Boulierac amesisitiza umuhimu wa kutoa huduma za elimu wakati wa mizozo.

Comments

Popular posts from this blog

VYOMBO VYA HABARI VINAWAJIBU WA KUELIMISHA JUU YA MALENGO 17 YA MAENDELEO ENDELEVU

DINI YAELEZWA KUWA KICHOCHEO CHA KUTIMIZA SDGS

7 hatua kuelekea maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030